Chama cha CUF jana kimezindua Kongamano la kudai Katiba mpya na Tume huru ya Uchaguzi, ikiwa ni siku 53 baada ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania kufanyika.
Chama cha CUF jana kimezindua Kongamano la kudai Katiba mpya na Tume huru ya Uchaguzi, ikiwa ni siku 53 baada ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania kufanyika.
Vilevile, amesema Rais anatakiwa kuheshimu ukomo wa Uongozi uliopo kwa mujibu wa Katiba na kuepuka majaribio yoyote ya kumuwezesha kukaa madarakani kwa muda mrefu.
Amesema Rais anapaswa kufufua mchakato ya kuandika Katiba mpya kuwapatia Watanzania Tume huru ya Uchaguzi itakayounganisha Taifa na kufuta machungu yaliyotokana na Uchaguzi Mkuu wa 2020.
Ameongezaa kuwa, rasimu ya Katiba mpya iliyo chini ya Jaji Mstaafu Joseph Warioba imekidhi matakwa ya wananchi walio wengi na jukumu alilobaki nalo Rais ni kuhitimisha mchakato huo.
Karibu tena Uhabarike katika ukurasa huu maalum na Rasmi wa gazeti bora na makini la kila siku la JAMVI LA HABARI. Tunayo furaha kukujuza kuwa JAMVI LA HABARI ndio gazeti linaloongoza kwa kuandika habari za kweli na umakini zilizochambuliwa na kufanyiwa utafiti wa kina. JAMVI LA HABARI, HAKIKA NI GAZETI LAKO.
Contact us: jamvilahabari@gmail.com