LAS VEGAS, MAREKANI
RAPA Cardi B atangaza kufuta akaunti yake ya Twitter mara baada ya kushindwa kuvumilia matusi ya mashabiki kuhusu kurudiana na mumewe Offset.
Card B alitangaza kujiondoa kwenye mtandao huo kupitia ukurasa wa Instagram akiwa LIVE (October 17) kwa kusema watu hawapaswi kuingilia maisha yake.
Wanandoa hao ambao walifunga ndoa mwaka 2017 na sasa wana mtoto mmoja, walirudisha mapenzi yao upya wiki iliyopita baada ya kusheherekea Birthday ya bibie huyo huko Las Vegas ambapo @offsetyrn alimzawadia Gari aina ya Rolls Royce siku hiyo